User:Robert Ullmann/Mwananchi/4 January 2009

User:Robert Ullmann/Mwananchi/header

amani
Bodi hiyo iliyoundwa na Meya ndiyo yenye jukumu la kusimamia utekelezaji suala hilo ikiwamo kuwatambua wafanyabiashara wenye sifa za kupangishwa, kusimamia amani na utulivu katika jengo hilo," alieleza. [1]
amri
Tunatoa amri kwamba shauri hilo lirudishwe Mahakama Kuu na lisikilizwe mbele ya jaji mwingine," jopo hilo limesema katika uamuzi uliosomwa na Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufaa, Profil Lyimo. [2]
anasema
Profesa Chris Peter Maina wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, anasema kuwa pamoja na serikali kuhusika kwa kiasi kikubwa katika vitendo vya uvunjifu wa amani, wananchi nao wanahusika kwa kiwango kikubwa. [3]
anaweza
Alisema kuwa katika hoja ya pili, Sheria ya Viapo, wakili anaweza kushuhudia kiapo. [4]
awali
Kwa mabadiliko hayo, mashtaka hayo sasa yatawahusisha watuhumiwa watatu badala ya wawili kama ilivyokuwa awali. [5]
bado
Tunaweza kwenda mahakamani, lakini bado viongozi tutalijadili kwanza. [6]
bali
Alisema watu wengi wanajidanganya kuwa mauaji haya hayawahusu, alisema mapambano hayo ni ya wote kwa sababu si mapambano ya kidini wala ya kikabila, bali ni mapambano ya kupigania haki za binadamu zinazovujwa huko Ghaza. [7]
bodi
SERIKALI imeiamuru bodi ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kuwachukulia hatua za kinidhamu wafanyakazi waliohusika katika uzembe uliosababisha shirika hilo kunyang’anywa leseni ya kurushwa ndege, huku ikitangaza mkakati wa kulihuisha. [8]
chake
Hadidu za rejea kwa hicho kikosi kazi alizitaja kuwa ni kuweka bayana matatizo ya ATCL, chanzo chake na kuishauri serikali hatua ambazo zinapaswa kuchukuliwa. [9]
chama
Lakini msaidizi wake, Zitto Kabwe ndiye aliyekuwa na kauli ya matumaini kwa wafuasi wa chama hicho kilichoibuka kidedea kwenye uchaguzi mdogo wa jimbo la Tarime. [10]
chini
Kwa sababu hiyo, alisema serikali imeamua kuunda timu ya watu saba, ambayo itakuwa chini ya makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Ardhi, Profesa Idrissa Mshoro ili kutoa tathmini ya kitaalamu. [11]
dakika
Hakimu Mwankenja alikubaliana na ombi hilo la upande wa mashtaka na akaahirisha kesi hiyo kwa muda wa dakika 15 ili kuipa mahakama nafasi ya kufanya tathmini upya. [12]
dola
Hata hivyo, ATCL ilirejeshewa cheti hicho Jumanne iliyopita baada ya kukamilisha kujaza kwa usahihi nyaraka hizo za TCAA. Serikali ilitoa dola 273,000 za Marekani kwa ajili ya kufanikisha zoezi la kusahihisha dosari zilizopkuwepo kwenye nyaraka muhimu za utoaji wa huduma za ndege. [13]
elimu
Haya yote yalitokana na tabia waliyoonyesha kiasi cha wananchi wa kawaida kabisa kuhoji uwezo, elimu na busara zao katika utendaji wao wa kazi. [14]
eneo
Mmbando alimkabidhi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Said Shaaban ambapo alimkabidhi hundi pamoja na seti za jezi na mipira 15 katika hafla fupi iliyofanyika ofisi za wizara hiyo zilizopo eneo la migombani mjini Zanzibar. [15]
es
Akitoa uamuzi kuhusu ATCL jijini Dar es Salaam jana, Waziri wa Miundombinu, Dk. [16]
fedha
Mganga alisema Mramba, ambaye wakati huo alikuwa waziri wa fedha, na Yona akiwa waziri wa nishati, waliingia mkataba huo kinyume cha Sheria ya Manunuzi ya Umma na Sheria ya Madini. [17]
hali
Hivyo ikagundulika kuwa kuna baadhi ya watu wanaokula rushwa kusajili wanafunzi kwa njia wanazojua na kuwapa namba za usajili bila kufuata utaratibu, hali ambayo inaharibu sifa ya chuo," alisema mtoaji habari huyo. [18]
hana
Kocha wa Zanzibar, Badr El Din alisema kwamba mchezo huo utakuwa mgumu na wachezaji hawatofautiani sana, lakini hana wasiwasi wowote. [19]
hao
Katika mashtaka hayo Mganga alisema washtakiwa hao kwa pamoja kati ya mwaka 2002 hadi 2005 wakiwa watumishi wa umma katika nafasi za uwaziri, walitumia vibaya madaraka yao kwa kuingia mkataba na kampuni ya M/S Alex Stewart (Assayers) Government Business Corporation ya Uingereza, ulioiwezesha kampuni hiyo kudhibiti uzalishaji wa madini nchini. [20]
hapa
Akichangia mjadala huo kwa kutoa mfano wa Cuba, afisa ubalozi wa Cuba hapa nchin, Dionisio Hernandez, alisema nchi za magharibi daima zimekuwa na sera za unyonyaji na njia pekee ya kujinasua ni kuwa na mshikamano isiotetereka. [21]
hasa
Alisema kama nchi za Afrika zikiungana na kuwa na msimamo wa pamoja katika mambo yake na hasa kuwa na soko la pamoja, itakuwa vigumu kuingiliwa na mataifa tajiri kwa kutumia ubaguzi wa watu wachache wenye uchu wa madaraka. [22]
hata
Akizungumza baada ya Maandamano ya kupinga hayo katika Uwanja wa Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam, Profesa Haroub alisema Rais Kikwete anayo nafasi ya kuwashawishi wakuu wa nchi za Afrika kulaani mauaji hayo kwa kuvunja uhusiano na Waisraeli na hata kuvunja uhusiano wa kubiashara na kiuchumi na nchi hiyo. [23]
hati
Kutokana na hatua hiyo, upande wa mashtaka, ambao jana uliongozwa na mwendesha mashtaka wa serikali, Biswalo Mganga umefanya mabadiliko katika hati ya mashtaka ya Mramba na Yona. [24]
hawa
Bila ya kupambana na uhalifu, wananchi watakosa amani kwani usalama wao na mali zao vitakuwa rehani, lakini sasa wanachokifanya hawa mgambo kukamata watu ovyo na kuwapiga hakiwezi kuungwa mkono. [25]
hayo
Alisema kifungu cha 38 (3) (a) katika Sheria ya Uchaguzi ya mwaka 1985 kinaeleza kuhusu wagombea ubunge pekee, hivyo kutokana na maelezo hayo jibu ni dhahiri kuwa sheria za viapo haziwezi kutumika katika viapo vya ubunge. [26]
hii
Kutokana na maelezo ya majibu ya hoja zilizoanishwa na kwa kuzingatia uamuzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika rufaa ya Ernest Binna mgombea ubunge jimbo la Bunda kwa tiketi ya CUF katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, Tume ya Taifa ya uchaguzi inakataa rufaa hii," alisema. [27]
hilo
Kauli yake ililingana na ya katibu wake mkuu, Wilbroad Slaa ambaye alilitazama suala hilo kisheria zaidi. [28]
hivi
Moja ya mambo yatakayofanyika katika marekebisho ya mkataba huo ni kuangalia uwezekano wa serikali kuwa na mamlaka katika suala la utawala ndani ya TRL... hivi sasa mamlaka yote yapo chini ya Kampuni ya Reli ya India (Rites)," alisema. [29]
hiyo
Lakini jana, mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji Lewis Makame aliwaambia waandishi wa habari kwenye hoteli ya Mount Livingstone kuwa baada ya kutafakari mambo makuu manne, tume yake imetupilia mbali rufaa hiyo. [30]
hizi
Hisia hizi za wasiwasi zimekuwa zikizidi kila siku kufuatia matendo yanayofanywa na askari hawa ambao wengi wao ni vijana ambao kwa hali ilivyo inaonekana wanmekosa moyo wa ubinadamu. [31]
hizo
Alisema kuwa ili kuweza kupata majibu ya hoja hizo, tume ilichambua kila hoja na kwamba katika hoja ya kwanza, tamko la mrufani (Shitambala) lililotolewa kwenye fomu zake za uteuzi halikuwa halali kwa kuwa alilifanyia kwa wakili. [32]
huko
Hivyo ni wakati sasa kwa Wafrika kuunga kupiga vita unyama na udhalimu unaofanywa na Waisrael huko Ghaza. [33]
huku
Mramba sasa anakabiliwa na mastaka 12 badala ya mashtaka 13 ya awali, huku Mgonja akikabiliwa na mashtaka nane kama ilivyokuwa awali, wakati Yona naye anakabiliwa na mashtaka matano kama ilivyokuwa awali. [34]
huo
Mgombea huyo hakukubaliana na uamuzi huo na kukata rufaa Tume ya Taifa ya Uchaguzi. [35]
huu
Waziri Kawambwa aliongeza kwamba bado wako kwenye majadiliano na RITES yaliyoanza mwezi Novemba mwaka jana na watakutana tena Januari mwaka huu. [36]
huwa
Kila mwaka ifikapo Januari mosi, maneno mengi husemwa kuhusu kampeni hiyo ya upandaji miti inavyoendelea, lakini baada ya tarehe hiyo kupita, na maneno hayo hupotea hadi Januari mosi nyingine au tarehe nyingine ambayo mkoa huwa umejipangia. [37]
ina
Ingawa serikali pia ina hisa ya asilimia 49 katika kampuni hiyo, tatizo liko katika mkataba wa uwekezaji kwani moja ya kipengele katika mkataba huo unairuhusu RITES kuajiri wafanyakazi na katika marekebisho haya moja ya maeneo yatakayotazamwa ni suala la menejimenti ya TRL ambayo kwa sasa ina wafanyakazi wote kutoka India. [38]
jeshi
Hata hivyo, serikali inalaumiwa kwa kulihusisha jeshi la polisi katika mambo ambayo jeshi hilo halikupaswa kushirikishwa moja kwa moja. [39]
jiji
Zungu ambaye ni mbunge wa jimbo la Ilala, alisema mamlaka ya kusimamia jengo hilo yako katika bodi iliyoundwa na Meya wa jiji na hakuna mtu yeyote aliyekasimiwa mamlaka hiyo hata awadanganye. [40]
jinsi
Ni kwa jinsi hiyo tu, kampeni ya upandaji miti inaweza kufanyika kwa ufanisi badala ya kuwa ya maigizo ya Januari mosi. [41]
juu
Alikuwa akitoa uamuzi wa serikali baada ya kupokea maelezo ya mwenyekiti wa bodi ya ATCL, Balozi Mustapha Nyang’anyi aliyotakiwa kuyatoa katika muda wa siku saba juu ya sababu zilizosababisha shirika hilo kunyang’anywa cheti hicho na TCAA Desemba 8, mwaka jana. [42]
kabisa
Tutafungwa na timu zote unazozijua, lakini si Bara hatukubali kabisa na wala hawawezi kufanya kitu kama hicho. [43]
kazi
Alisema kuwa kutokana na siku hizo wagombea walikuwa na siku sita za kazi ambazo wangeweza kuzitumia katika kuwasilisha viapo vyao kwa mahakimu kwani mrufani alijua wazi kuwa siku za sikukuu na mwisho wa wiki mahakama hazifanyi kazi hivyo alitakiwa kuchukua tahadhali kwa kutumia siku ambazo mahakama zinafanya kazi. [44]
kesi
HATIMAYE katibu mkuu mstaafu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Gray Mgonja jana aliunganishwa katika kesi inayowakabili mawaziri wa zamani, Basil Mramba na Daniel Yona ya matumizi mabaya ya ofisi za umma na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya Sh11 bilioni. [45]
kiasi
Mashtaka mengine kwa washtakiwa hao ni kutoshughulikia suala la ada ya madini na kutopeleka makubaliano kwa mwanasheria mkuu wa serikali na hivyo kuipa kampuni hiyo muda wa nyongeza kabla ya kushughulikia suala la kiasi cha ada ambacho kampuni hiyo ilitakiwa kulipa. [46]
kifungo
Mtu anaweza kuwekwa chini ya ulinzi au kifungo kisicho halali kutokana na sababu mbili au zaidi. [47]
kike
Sheria ya Makosa ya Kujamiiana ya mwaka 1998, pamoja na mambo mengine, imelenga kuthibiti unyanyasaji wa kijinsia ukiwemo kuwapa mimba watoto wa kike lakini haijafanikiwa kwa kiwango kilichotarajiwa licha ya ukali wake. [48]
kituo
Hata hivyo; waandaji wa mchezo huo walikuwa hawajaripoti kituo chochote cha Polisi kwa ajili ya kuchukua hatua za kuwasaka waliohusika na tukio hilo ambalo si la kimichezo. [49]
kocha
TIMU za Tanzania, Zanzibar na Kilimanjaro Stars leo zitashuku dimbani kwenye uwanja wa Nakivubo kwa nyakati tofauti, huku kocha Marcio Maximo akiwatahadhalisha :"wachezaji wake atayecheza chini ya kiwango katika mashindano haya ya Chalenji tusilaumiane. [50]
kujua
Wanafunzi hao walipeleka malalamiko yao kwa uongozi wa serikali ya chuo wakitaka kujua sababu za kutokuwa na sifa za kujiunga na chuo hicho wakati walishafanya majaribio. [51]
kuna
Bado kuna namna ya kufanya. [52]
kupiga
Profesa Haroub Othman wa chuo hicho, alisema umefikia wakati kwa Waafrika kuonesha mshikamano kupiga vita unyama wanaofanyiwa Wapalestina kwani mapambano yao ni mapambano ya Afrika kwa sababu wote wanapinga vita na ubeberu. [53]
kusema
Tunajidanganya kwa kusema kuwa mauaji haya hayatuhusu. [54]
kuu
Morogoro kupitia soka na kuwataka wasibweteke na ushindi huo bali wajitahidi kufanya vizuri katika ligi kuu inayotarajia kuanza baada emwezi huu. [55]
kuuaga
Kumbi mbalimbali za burudani zilifulika watu katika hekaheka za kuuaga mwaka na kuukaribisha mwaka mpya huku kuwa na matukio ya kufurahisha na kuburudisha. [56]
kuwapa
Mbali na uamuzi huo, serikali pia imeamua marekebisho ya mkataba wa uwekezaji wa Kampuni ya Reli (TRL) ili kuwapa Watanzania nafasi ya kuingia katika bodi ya wakurugenzi na kuwemo kwenye menejimenti. [57]
kwa
Mgombea wa Chadema, Sambwee Shitambala alienguliwa na Tume ya Uchaguzi ya Mbeya Vijijini baada ya vyama vya CCM na CUF kuwasilisha pingamizi, vikidai kuwa alikiuka Sheria ya Uchaguzi kwa kuapa kwa wakili badala ya kwa hakimu. [58]
la
Kwa kuwa suala hili ni la kisheria, ni vema ukatupa muda kwanza ili tulijadili kuona tutafanyaje," alisema Dk. [59]
lake
Katika ziara hiyo Nnauye aliwapa wazee hao zawadi ya vikombe vya kahawa, birika lake na fedha taslimu Sh100,000 kama ishara ya kuwataka waendelee kukutana kwenye shina hilo na kuzungumza mambo ya chama. [60]
ligi
Tunajua Tanzania ni timu ngumu na ina wachezaji wengi wa viwango vya juu lakini njooni muone mpira,kwenye kikosi chetu mimi mwenyewe ndio nacheza ligi wengine wote hawachezi sababu ya vita lakini kazi itafanyika. [61]
maisha
Naamini kwa kufanya hivyo, watabadilika na kusaidia katika utoaji wa elimu kwa wakazi wa jiji kuhusu haki na wajibu wao, ili sote tufurahia matunda ya nchi hii na kuendesha maisha kwa amani na kuheshimiana. [62]
mapema
Waziri Kawambwa alisema hatua hiyo inatokana na marekebisho ya mkataba ulioanza mapema mwaka jana baada ya serikali kuunda kamati ya kupitia upya mkataba huo. [63]
mara
Haiwezekani kila mara wawe chanzo au wahusishwe na vurugu. [64]
mengi
Maeneo mengine yaliyokuwa yanasheherekea usiku huo hapa nchini ni pamoja na Makumbusho,Vatcan City Sinza, Kempisk, Movenpik Hotel, New Msasani Club, Roya Zambezi Mbeya, Splended Tanga, Kibo Kigoma, Twisters Pub na maeneo mengine mengi hapa nchini. [65]
miti
JANA ilikuwa siku ya uzinduzi wa kitaifa wa mwaka wa zoezi la upandaji miti wakati Rais Jakaya Kikwete alipoongoza kampeni hiyo kandokando ya Barabara ya Kilwa. [66]
mkoa
MABINGWA wa Kombe la Tusker, Mtibwa Sugar ya Turiani mjini Morogoro, imewasili mkoani hapa na kupata mapokezi makubwa huku serikali ya mkoa ikiahidi kutoa sh 1 milioni kwa wachezaji wa timu hiyo. [67]
moja
Alisisitiza kuwa serikali ipo tayari kumuwajibisha yeyote iwapo atatajwa kwenye ripoti hiyo kwa kuwa lengo ni kuhakikisha ATCL inaondokana na wingu la vikwazo na kuwa moja ya mashirika makubwa ya ndege barani Afrika. [68]
mpya
Mgogoro huo ulichukua sura mpya mwezi Oktoba 8 mwaka 2001 baada ya halmashauri hiyo kutoa matangazo kwa vipaza sauti, ikiwataka wananchi hao waondoke katika ardhi iliyobaki ndani ya siku nne. [69]
mtu
Kwa kuwa tamko limesainiwa na mtu asiyehusika, ni dhahiri kuwa tamko hilo (la kiapo) si halali na ni sababu ya kuweka pingamizi iliyotajwa katika kifungu cha 40(1) (d) cha sheria ya uchaguzi Na. [70]
mzima
Walisema baada ya safari ndefu ya siku 360 za pilika pilika, kukamilika na kuanza safari zingine ni lazima kwa mtu kujipongeza kwa kuvuka mabonde na milima ya mwaka mzima. [71]
nao
Tanzania ina wachezaji wazoefu na mastaa, lakini mimi nina vijana wengi ambao nataka wafanye kazi, nimetoka nao mbali ndio maana nawaandaa kuwa mabingwa wa hii michuano mwakani. [72]
nayo
Naamini kwamba kila mmoja wenu anaweza ndio maana nikamjumuisha kwenye timu yangu ya ushindi, hii timu niliyokuja nayo ni kikosi cha kwanza na ndio timu yangu bora zaidi kwa hiyo nategemea mambo makubwa. [73]
nchi
WAHADHIRI waandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wamemtaka Rais Jakaya Kikwete kutumia nafasi yake ya uenyekiti wa umoja wa Afrika kuwashawishi viongozi wa nchi za Afrika kuunga mkono katika kupinga mauaji ya Wapalestina yanayofanywa na Israel katika ukanda wa Gaza. [74]
ndio
Jaji huyo alisema kwa kuwa katika kifungu cha 38 (3) kuna neno linaloonyesha kuwa hakimu wa mahakama ya mwanzo, wilaya na mahakama za hakimu mkazi ndio wanaopaswa kushuhudia tamko hilo la kiapo, ni dhahiri kuwa wakili hapaswi kushuhudia tamko mgombea ubunge. [75]
ndiyo
Pia kimewataka viongozi wa ngazi ya juu wa Chadema kukubali makosa yao kuwa ndiyo yaliyosababisha kufanyika kwa makosa wakati wa kiapo. [76]
ndoa
ATCL iliwahi kuingia ubia na Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA), lakini baadaye serikali iliona ndoa hiyo haina manufaa na kuamua kuivunja miaka mitatu iliyopita. [77]
nguvu
Siku nne baadaye, askari polisi walivamia kijiji hicho na kuwaondoa wanakijiji hao kwa nguvu kabla ya kuharibu mali na kuchoma nyumba zao moto. [78]
nje
Wafuasi wa Chadema hawakuweza kusogelea hoteli ya Mount Livingstone wakati Jaji Makame akitangaza uamuzi huo kutokana na kuwepo na ulinzi mkali wa maafisa wa usalama wa Jeshi la Polisi na Askari wa Kutuliza Ghasioa (FFU) waliokuwa nje ya geti la hotel hiyo. [79]
ombi
Hakimu Mwankenja alikubali ombi hilo. [80]
raia
Baada ya mchezo huo kocha wa Zanzibar, Badr el Din raia wa Misri alisema kwa sasa nategeneza timu ya kutwaa ubingwa mwakani, lakini nimefurahishwa na matokeo pamoja na kiwango tulichokionyesha kwa leo. [81]
saa
Jana Mramba na Yona walipanda kizimbani saa 5:20 na baadaye Wakili Mganga akaiomba mahakama Mgonja aunganishwe katika kesi hiyo. [82]
sasa
Siwezi kueleza chochote kwa sasa kwa sababu tunahitaji kufanya consultations (mashauriano)," alisema mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alipotakiwa kuzungumzia hatua inayofuata baada ya Jaji Makame kutangaza uamuzi huo. [83]
sifa
ZAIDI ya wanafunzi 1,000 wa mwaka wa kwanza kwenye Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) wamegundulika kuwa hawana sifa za kujiunga na chuo hicho. [84]
sisi
Walisema kitendo cha kuwaita kwenye kamati ya nidhamu na kuwatuhumu kuwa wao ndio wanaohamasisha watu kugoma wakati sisi wanafunzi ndio wanaowatuma kuwatetea, ni kuwakandamiza. [85]
timu
Enrigue Sagura wa kampuni hiyo kushiriki katika kikao na kuiongezea kampuni hiyo muda wa nyongeza wa miaka miwili kabla ya majadiliano ya timu ya wataalamu wa serikali. [86]
umri
Wapo walionaswa wakiwapiga wananchi viboko hadharani bila hata ya kujali umri na hadhi yao katika jamii. [87]
uwezo
Jaji Projest Rugazia wa Mahakama ya Ardhi alitupilia mbali ombi hilo baada ya kuridhia pingamizi la awali lililowekwa na wajibu maombi kwamba mahakama hiyo haikuwa na uwezo wa kisheria kushughulika na shauri hilo. [88]
viapo
Lakini akaongeza kuwa Sheria za Viapo zinahusu viapo na matamko ya kisheria kwa ujumla. [89]
wa
VIONGOZI na wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana waliachwa wakitafakari cha kufanya baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutupilia mbali rufaa ya mgombea wao kupinga kuenguliwa kwenye kinyang'anyiro cha ubunge wa Mbeya Vijijini. [90]
wale
Shukuru Kawambwa alisema kuwa wafanyakazi wanaopaswa kuwajibishwa ni wale ambao walizembea wajibu wao, hivyo kuisababishia serikali hasara kubwa. [91]
walimu
Utafiti pia umebaini upungufu mkubwa wa walimu. [92]
watu
Tumegundua kuwa mapungufu yapo maana kuna watu ambao wanahusika katika kuhakikisha kuwa ndege za ATCL zinaruka," alisema Dk. [93]
wazee
MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (Nec) Nape Nnauye, amekemea makundi ndani ya chama hicho na kuwataka wazee kutumia nafasi yao ya Kikatiba kuonya na kushauri ili chama kirudi katika misingi yake. [94]
wenyewe
Hapa sababu kubwa huwa ni raia wenyewe. [95]
wote
Kuhusu hoja ya wagombea kama walikuwa na muda wa kutosha wa kukamilisha fomu zao za uteuzi na kuziwasilisha kwa wakati, Jaji Makame alisema kuwa kwa mujibu wa barua ya msimamizi wa uchaguzi ambayo walipatiwa makatibu wote wa vyama vya siasa wa wilaya, wagombea walitakiwa kuchukua fomu za uteuzi kuanzia Desemba 17,2008 hadi Desemba 27,2008 ambayo ilikuwa siku ya kwanza. [96]
yao
Katika mabadiliko hayo kwenye hati ya mashtaka ya kesi hiyo namba 1200 ya mwaka 2008, Mramba ambaye ni mshtakiwa wa kwanza amepunguziwa mashtaka wakati Yona, ambaye ni mshtakiwa wa pili, na Mgonja ambaye ni mshtakiwa wa tatu, wanaendelea kukabiliwa na mashtaka yao ya awali. [97]
yetu
Tumesikiliza matokeo ya rufaa yetu ambayo Tume ya Taifa imetupilia mbali, tunahitaji muda wa kutafakari kwa undani. [98]
yote
Kawambwa alisema kuwa tayari serikali imefuta madeni yote ya ndani ya ATCL na imeridhia kutoa Sh3.3bilioni kama sehemu ya kuanzia katika kulisuka upya shirika. [99]
za
Alisema hoja ya pili ni kama Sheria za Viapo (Oaths and Statutory Declarations Act, Cap 34 R.E 2002 na Notaries Public and Commissioners for Oaths Act, Cap 12 E.R. 2002) zinaweza kutumika katika suala hili na kama wagombea walikuwa na muda wa kutosha wa kukamilisha fomu zao za uteuzi na kuziwasilisha kwa wakati. [100]